Tyga akanusha tetesi za kuwa na uhusiano na Kylie Jenner (mdogo wa Kim K) mwenye miaka 17
Baada ya rapper Tyga kuachana na baby mama wake Blac Chyna miezi miwili iliyopita, kuna tetesi kuwa rapper huyo ameanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi na mdogo wake Kim Kardashian aitwaye Kylie Jenner mwenye miaka 17.
Lakini kama ilivyo kawaida ya mastaa wengi, Tyga (24) amekanusha kwa kusema tetesi hizo si za kweli, na kusisitiza kuwa hana uhusiano wowote na mtoto huyo mrembo Kylie, zaidi ya urafiki wa kawaida alionao na familia yao.
“DON’T BELIEVE THE RUMORS, BEEN FRIENDS WITH THE FAMILY FOREVER. WERE [sic] ALL JUST FRIENDS,” Alitweet Tyga.
Blac Chyna alikuwa rafiki mkubwa wa Kim Kardashian kiasi cha kufanya familia zao ziwe na ukaribu.
Kylie
Tetesi za Tyga na Kylie kuwa wapenzi zimeedelea kupata nguvu zaidi wiki hii baada ya wawili hao kuonekana wakipata dinner kwa mara ya pili katika mgahawa mmoja wa Kijapan huko Hollywood Jumatatu wiki hii. Hii ni baada ya kuonekana kwenye dinner ya kwanza wiki iliyopita huko Sherman Oaks.
Tyga na Kylie wakitoka dinner
Wakati bado mambo hayajapoa Tyga alipost picha nyingine jana akiwa na Kylie na Big Sean.
Tyga, Kylie na Big Sean
US Weekly pia iliripoti kuwa Tyga na Kylie wamekuwa wapenzi wa siri toka mwezi wa nane toka Tyga alipotengana na Blac Chyna.