Burudani

Tunda Man akanusha kuwahi kuwa na uhusiano na Wema wala Nyota Ndogo

Msanii wa muziki, Khalid Ramadhani maarufu kama ‘Tunda Man’, amedai kuwa hajawahi kuonja penzi la Wema Sepetu na wala hana mpango huo.

Tundaman

Akizungumza na Global TV, Tunda amesema haendani na Wema.

“Hamna kitu kama hicho, mimi kama kapteni wa Bongo FlAVA sijawahi kulionja hilo penzi. Ni mshikaji wangu tu, kweli kabisa ni mshikaji wangu tu ambaye ‘mambo poa’, ‘post hii picha’ napost. Kuna kipindi alikuwa karibu na sister yangu Snura tukawa karibu sana. Mimi binafsi sitamani Sepetu awe mpenzi wangu, sitamani kabisa yaani kwa sababu nahisi kuna vitu tutakuwa tunapishana. Mimi nikaenda kulia na yeye akaenda kushoto na hizi ngumi tunazocheza ninaweza piga mpaka nikaua. Mimi najua Sepetu ni shemeji yangu najua namrespect kama shemeji yangu,” alisema Tunda.

Pia katika hatua nyingine Tunda amekanusha kuwa na mahusiano na msanii wa Kenya, Nyota Ndogo.

“Nyota Ndogo ni kama sister yangu, rafiki yangu,” alisema. “Kipindi naenda Mombasa nilikuwa na show mbili, kuna sehemu moja inaitwa Kilifi na nyingine ni boda ya Mombasa na Moshi, kwahiyo ukisikia naenda huko lazima upite kwao na huwaga ananipigia simu kama utapita huku pitia hapa uje ule nini! Basi tukapita pale na team yangu akatupikia tukala tukapiga piga picha. Lakini zile picha ambazo zilikuwa zinapigwa ni mikao ya kisanii ambayo imewachanganya watu. Hakuna lolote na kuna ngoma yake nimefanya kwahiyo tunashare vitu kama wasanii.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents