Picha

Trump kuwatimua wahamiaji haramu milioni 3 kutoka Marekani

Wasiyemtaka ameingia ikulu ya Marekani na kama walikuwa wakidhani vitisho alivyokuwa akivitoa wakati wa kampeni vilikuwa ni mkwara tu, wanapaswa kujipanga upya!

3a550df400000578-3932048-image-a-63_1479054448084

Ni kwasababu Rais Mteule wa nchi hiyo, Donald Trump ameusisitizia msimamo wake dhidi ya wahamiaji haramu nchini humo. Amedai kuwa ana mpango wa kuwafungashia virago wahamiaji haramu takriban milioni tatu,hasa wale wenye rekodi ya uhalifu.

Amesisitiza pia kuwa mpango wa kujenga ukuta upo pale pale.

Katika mahojiano yake ya kwanza tangu ashinde uchaguzi na kuja kuchukua kijiti cha Urais toka kwa Barack Obama, Trump amewahakikishia wafuasi wake kuwa atawatimua wahuni na wauzaji wa madawa ya kulevya wote toka Marekani.

3a550e2800000578-3932048-image-a-67_1479054464747

Katika mahojiano kwenye kipindi cha CBS, 60 Minutes, Jumapili jioni, Trump amesema atajenga ukuta kutenganisha Mexico na Marekani kama alivyoahidi kwenye kampeni yake.

3a50aec800000578-3932048-image-a-11_1479055968201

Kuna wahamiaji haramu takriban milioni 10 nchini Marekani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents