Burudani
Trey Songz kutumbuiza kwenye tuzo za MTV MAMA, ataungana na Miguel na French Montana
MTV Base imetangaza kuwa muimbaji wa RnB, Trey Songz atatumbuiza kwenye tuzo za MTV Africa Music (Awards) 2014.
Host wa show hiyo atakuwa mchekeshaji na muigizaji wa filamu Marlon Wayans. Tuzo hizo zitafanyika kwenye ukumbi wa ICC, Durban June 7 ambapo pamoja na Trey wasanii wengine kama Miguel, rapper French Montana, Davido, Flavour, Tiwa Savage, and Mafikizolo, Uhuru, Oskido na Professor watatumbuiza.
Diamond ametajwa kuwania tuzo mbili mwaka huu.