Burudani

TID asema alikuwa anatoka kimapenzi na Wema lakini akatemwa

Msanii mkongwe wa muziki, TID amesema kipindi cha nyuma alikuwa anatoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu lakini baadae alitemwa hali ambayo ilimuumiza sana.
TID

Akizungumza katika kipindi cha Clouds TV Ijumaa hii, TID amesema hali hiyo ilimfanya atoke na wasichana wengi.

“Nilikuwa ‘namdate’ Wema Sepetu akaniambia sikutaaki, tangu kipindi hicho nimekuwa na wasichana wengi. Ikitokea Wema anataka kurudi hakuna nafasi, I’m occupied,” alisema TID.

TID amesema katika kipindi hicho aliumizwa sana na jinsi magazeti yalivyokuwa yanamuandika vibaya.

“Wakati huo mitandao ya kijamii haikuwepo lakini wamagazeti walizichukua picha na kufanya yao, it was bad. Mimi nikasema sawa lakini niliumia sana,” alisema TID.

Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Confidence’ aliyomshirikisha Joh Makini pamoja na Dully Sykes.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents