Burudani

Thamani ya gauni la Beyonce alilovaa kwenye NBA All-Star, lazima uumwe

Je unajua thamani ya gauni alilovaa Beyonce Jumapili iliyopita kwenye kwenye mchezo wa NBA All-Star Game? Ukisikia thamani yake utashangaa.

Gauni hilo ambalo limetengenezwa na kampuni ya Gucci linafahamika zaidi kwa jina la Gucci Kimono lina thamani ya kiasi cha dola 21,945 ambapo kwa fedha za kitanzania ni zaidi ya shilingi 44,000,000.

Mara kadhaa Queen Bey na familia yake wamekuwa wakivaa nguo zinazotengenezwa na kampuni hiyo. Hata wiki iliyopita kwenye tuzo za 59 za Grammy mtoto wake Blue Ivy alivalia koti la suti lenye rangi ya pink lililotengenezwa na kampuni ya Cucci.


Blue Ivy akiwa na baba yake Jay Z wakati wa tuzo za 59 za Grammy Jumapili iliyopita

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents