Bongo MovieUmbea
Tetesi mtaani: Mwigizaji Lulu ana ujazito wa kigogo wake?!
Inasemekana kwamba mwigizaji nyota wa Bongo Movie Lulu ni mja mzito, mrembo huyo ambaye alikabiliwa na kashfa ya kuhusishwa na kutembea na Kigogo mmoja na kusadikiwa kwamba amejengewa nyumba baada ya kumpagawisha kigogo huyo lakini taarifa zaidi kutoka kwa mtu wake wa karibu zinasema kwamba kisa cha kigogo huyo kumjengea nyumba hiyo ni kutokana na binti huyo kumbebea ujauzito.
Taarifa hizo za mtu wake wa karibu zinasema kigogo huyo ambaye kiumri ni mtu mzima, inasadikiwa amekolea kiasi cha kumjengea nyumba ya gharama.
Mwandishi wa Bongo5 alijaribu kuwasiliana naye, lakini simu ya binti huyo ilikuwa haipatikani na hata hivyo tutaendelea kumtafuta na kuona ni kweli kama kwa sasa anatarajia kupata mtoto.