Temba kusherehekea siku ya kuzaliwa leo kwa kufanya show itayokusanya pesa kusaidia watoto
Msanii wa muziki Mh Temba leo anatarajia kufanya show ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, itakayofanyika kwenye ukumbi wa Ikweta Grill Temeke, ambapo mapato yatakayopatikana yatapelekwa katika wodi ya watoto katika hospitali ya Temeke.
Akizungumza na Bongo5 leo, Fella amesema Temba atasindikizwa na wasanii mbalimbali wakiwemo waimbaji wa taarab.
“Maandalizi yapo tayari burudani itakuwa kubwa kwa sababu licha ya kuwepo kwa Wanaume Family, Dogo Janja, Isha Mashauzi pamoja na Yamoto Band wote watakuwepo kuhakikisha burudani inaenda vizuri. Kwakuwa hii ni burudani kwajili ya Mh Temba kusherekea siku yake ya kuzaliwa baadhi ya mapato yatakayopatikana yatapelekwa katika wodi ya watoto katika hospitali ya Temeke, kwa hiyo tunaomba wadau watuunge mkono kwenye hili,” alisema Fella.