Technology

Teknolojia: China kutengeneza ‘lifti’ yenye kasi zaidi duniani inayoweza kupanda ghorofa 95 kwa sekunde 45

Kampuni ya Hitachi imetangaza mpango wake wa kutengeneza lifti yenye kasi zaidi duniani (The world’s fastest ultra-high-speed elevator) katika jengo refu la Guangzhou CTF Finance Centre linalojengwa huko Guangzhou, China.

CTF1
Mchoro wa jengo hilo refu la Guangzhou CTF

Jengo hilo linalotazamiwa kukamilika ifikapo mwaka 2016, litakuwa na lift hizo zenye uwezo wa kwenda kasi ya kupanda au kushuka ghorofa 95 kwa sekunde 45.

Hitachi wamesema lifti hizo zitatumia teknolojia ambayo inahakikisha usalama kwa watumiaji, hivyo wasafiri watakuwa wakisafiri salama na kwa raha pamoja na mwendo wake mkali.

CTF2
Ujenzi wa kikwangua anga hicho cha CTF ulianza mwaka 2010 na picha hii ilipigwa 23 December 2012, na linatarajiwa kukamilika mwaka 2016.

Source: Daily Mail

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents