Burudani
Tanesco wataja kiasi wanachomdai Wema Sepetu kufuatia kuiba umeme!
Tanesco wako shingoni kwa Wema Sepetu!
Hivi karibuni walifanya ziara ya kushtukiza kwenye nyumba yake na kubaini kuwa muigizaji huyo anatumia umeme wao bure!
Jana Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Eng. Felichesmi Mramba alizungumza na waandishi wa habari na kutaja kiasi cha fedha kitakachopatikana kutokana na faini waliyowapiga wezi mbalimbali wa umeme.
Imebainika kuwa Wema Sepetu anadaiwa shilingi 8,200,496.20.