Tamasha la Manywele laja kivingine
Muungano kati ya Mnywele Entaiment na Africans Stars Entetaiment wamiliki wa bendi tya Twanga Pepeta, wanatarajia kufanya bonge la tamasha la kuizindua upya Tamasha la Manywele Kimwana wa Twanga Pepeta litakalo fanyika May 6, pale Club Sunciro.
Akiziungumza na mwandishi wa Bongo5, Maimath wa Jesse alisema tamasha hioli kwa mara ya kwanza lilifanyika mwaka 2003, na baadaye kupotea wakati huo lilikuwa likiitwa Miss Twanga.
Anasema kwa sasa wamepata wanawake 23, wa kuanzia miaka 18 hadi 36 awe ameolewa au hajaolewa, awe anafanya kazi au hafanyi kazi, ambapo mshindi atazawadiwa duka la vipodozi lililopo Studio Kinondoni, pia na kugewa elimu ya Ujasiliamali.
Aidha amedai kwamba mwaka huu wamefanya mabadiliko makubwa katika zawaidi ilikwenda sawa na msemo wa kauli yao ya ‘Tumwinue Mwanamke’ na kumwezesha mwanamke katika maendeleo ya Sayansi na kujitegemea kiuchumi.
Amesema hii pia ni changamoto kwa wanaume iliwaweze kusaidia katika Taasis mbalimbali, ilikuweza kumsaidia mwanamke katika maendeleo ya leo.
Maimath akiwa na Husna Kimwana 2007 maarufu kama Sajet wakiwa kwenye flemu ya duka ambalo litakuwa zawadi ya Mshindi wa Manywele Kimwana wa Twanga