Habari
Taliban wathibitisha kifo cha kiongozi wake Mullah Akhtar Mansoor, wamteua huyu kurithi nafasi yake
Kundi la kigaidi la Taliban la nchini Afghanistan, limethibitisha kifo cha kiongozi wake mkuu, Mullah Akhtar Mansoor aliyeuwa na ndege za Marekani wiki iliyopita.
Picha iliyotolewa na Taliban kumuonesha kiongozi wake mpya Mullah Haibatullah Akhundzada
Pia limemteua mrithi wake.
Mullah Haibatullah Akhundzada, msomi maarufu wa dini na aliyekuwa msanii wa kiongozi huyo ataliongoza kundi hilo. Kundi hilo lilipata pigo zaidi baada ya muasisi wake Mullah Omar kupoteza maisha mwaka jana.