Michezo
Steven Adams kuiweka nafasi ya Hasheem Thabeet Oklahoma City Thunder matatani?
Steve Adams, ni mchezaji mpya kutoka New Zealand aliyechukuliwa kwenye ligi ya NBA mwaka jana na timu ya Oklahoma City Thunder anayoichezea Mtanzania, Hasheem Thabeet.
Steve Adams
Alisainishwa na timu hiyo July 12, 2013, November 8, 2013, alifanikiwa kufunga point 17, rebounds 10, assists 2 na kuzuia blocks 3. Tangu ajiunge na Oklahoma City, amekuwa na wastani wa point 3.8 na rebounds 4.6.
Hasheem Thabeet
Kutokana na uwezo wake katika nafasi ya kati amegeuka kuwa backup muhimu na kumshinda Hasheem Thabeet kwenye nafasi hiyo.