Bongo Movie

Steve Nyerere amkabidhi Mama Maria Nyerere Zawadi ya Movie

Mwigizaji wa filamu nchini Steve Mangele ‘Steve Nyerere amekabidhi filamu yake ya Mwalimu Nyerere kwa mke wa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere ikiwa kama shukrani zake,baada ya mama huyo kumsaidia katika kukamilisha filamu hiyo ambayo aliifanyia Butiama.
Steve alisema kwamba kumpa filamu hiyo ni kuweka kumbukumbu kwamba, anathamini msaada na mchango wake katika filamu hiyo na hana kikubwa cha kumpa wala cha kumfanyia zaidi.
Amesema, Mama Maria Nyerere alimsaidia sana kujifunza mengi kumhusu baba wetu wa taifa ikiwemo kumuonyesha vitu gani Mwalimu alikuwa akifanya, na vitu gani mwalimu alikuwa akivipenda,na hata na sehemu ambazo mwalimu alipenda kukaa baada ya kazi zake.
Pia ametoa shukrani kwa wasanii wenzake ambao walijitahidi katika hali moja au nyingine kuhakikisha filamu hiyo ilikamilika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents