Burudani
Stamina: Siwezi kufanya video ya gharama kubwa
Msanii wa Hip Hop, Stamina amedai kuwa kamwe hatofanya video ya gharama kubwa wakati muziki wake bado unamlipa pesa kidogo.
Stamina ameiambia Bongo5 kuwa kipato anachopata kwenye muziki hakijamshawishi kufanya video ya gharama kubwa.
“Kwanza siwezi kufanya video ya gharama kubwa hilo sahau,” amesema. “Yaani kusema nifanye video ya milioni 80 wakati nachokiingiza hakipo hivyo. Kwanza sina management, sina promoter. Maisha yangu naendesha mimi kama mimi na muziki wangu, cha msingi ni kufanya video kali, video ya ‘Uko Kwenu Vipi’ inakuja pia kuna video ya wimbo mpya inakuja kwahiyo watu waendelee kusubiri muziki mzuri.”