Spice Girls kuungana tena, waingia studio kurekodi nyimbo
Kundi la akina dada lililowahi kutamba duniani, Spice Girls linaungana tena. Member watatu kati ya watano wameingia studio kutengeneza kazi mpya.
Geri Horner (Ginger Spice), Melanie Brown (Scary Spice) na Emma Bunton (Baby Spice) walitumia saa 40 kwenye studio za Play Deep jijini London kurekodi nyimbo mpya huku wakipanga kuachia album mpya baadaye mwaka huu kusherehekea miaka 20 tangu watoe album yao ya kwanza, Wannabe.
Pia mwaka 2017 watafanya show za live katika maeneo mbalimbali. Jumatano hii Mel B alipost picha Instagram akiwa na wenzake hao wawili na kuandika, “And I say oohhhh LALA.”
Hata hivyo Victoria Beckham (Posh Spice) hatohusika huku pia Mel C (Sporty Spice) hakuwepo kwenye studio za Play Deep baada ya mapema mwaka huu kudai kuwa atafanya muziki mwenyewe.
Wamewahi kuungana tena kwa muda mfupi mwaka 2007 na 2012.