Michezo

Southampton yatinga fainali ya EFL kwa kuifunga Liverpool

Klabu ya soka ya Southampton imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya kombe la ligi zamani likijulikana kama Capital One baada ya kuifunga Liverpool kwa jumla ya mabao 2-0 katika michezo miwili waliyoicheza.

Katika mchezo wa nusu fainali ya pili ya kombe hilo uliofanyika usiku wa Jumatano hii, Liverpool walikuwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Anfield na walifungwa 1-0 na Southampton kwenye dakika ya 90 huku goli hilo likifungwa na Shane Long.

Wakati huo huo katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza uliochezwa Januari 11 mwaka huu katika uwanja wa St. Mary’s unaomilikiwa na Southampton walifanikiwa kuifunga Liverpool kwa bao 1-0 kupitia kwa mchezaji wake Nathan Redmond.

Sasa timu hiyo inamsubiri mshindi katika fainali itakayochezwa kwenye uwanja wa Wembley Februari 26 kati ya Manchester United na Hull City ambao wanacheza nusu fainali yao ya pili Alhamisi hii huku mechi kwa kwanza Man United ilifanikiwa kushinda maba 2-0.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents