Burudani

Sio Dimpoz tu, Wema, Shetta, Choka, Ray, Shilole, BASATA nao ni wahanga wa ngoma mpya ya Nay wa Mitego

Nay wa Mitego amechafua hali ya hewa tayari.

12534376_937830476307673_1527161113_n

Wimbo wake mpya Shika Adabu Yako umejaa controversy kibao.

Ommy Dimpoz amejibu tayari kwa kile alichoambiwa. Soma hapa.

Lakini kuna wahanga zaidi ya Ommy. Wapo pia Wema Sepetu, Shetta, DJ Choka, Ray, Shilole na hata BASATA. Hii ni baadhi ya mistari yenye utata:

Bongo Movie imekufa wamebaki kuuza sura
Wote wanataka kuimba ka Shilole na Snura
Ray Kigosi kawa mkongo hadi leo anaishi kwao
Hela za kuuza movie zote ananunua mkorogo
Kama ni umri umeshaenda, au bado anajiona dogo?

Kama ni vumbi litaruka na mikia watafyata
Hizi taarifa zangu na ziwafikie BASATA
Nyie ni kuku au bata? Msumeno usiokata
Kazi kufungia nyimbo, mnajua shida tunazopata?
Hamjui wajibu wenu, mngekuwa watoto nshawachapa

Na wasanii wadananda, ila Shetta kazidi
Huyo ndo baba Qaila (okay!)
Gari kapewa na Chief Kiumbe utasikia, “my new ride!”

Huyu jamaa anajiita Dimpoz, Poz kwa Poz
Wanae wanalalamika hawamjui shemeji
Kitaani kuna tetesi mwana hapigi mechi
Mara oh jogoo hawiki, huwa haonyeshi shemeji

DJ Choka daily bata, hivi hauna familia?
Nasikia hata nyumbani huna godoro la kulalia

Wema Sepetu una mimba kweli, au ndo kiki za msimu?
Miezi tisa sio mingi, isije ikakugharimu
Na siku hazigandi tayari ushakuwa bibi
Na unakoelekea utatafuta kiki hadi kwa Fid

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents