Burudani
Single mpya ya Queen Darleen ‘Wanatetemeka’ aliyomshirikisha Shilole kutoka rasmi wiki hii, atumia beat ya ‘Nakomaa na Jiji’
Msanii wa kike Queen Darleen anatarajia kuachia single yake mpya kwa mwaka huu 2014 aliyomshirikisha Shilole, wimbo ambao umetumia beat ya ‘Nakomaa na Jiji’.
‘Wanatetemeka’ ndio jina la single mpya ya Darleen ambayo imefanyika katika studio ya Mazuu chini ya producer Mazuu huku ikitumia beat ya wimbo uliopita wa Shilole ‘Nakomaa na Jiji’.
Akiongea na Bongo5 Guru a.k.a G-Lover amesema single hiyo itaanza kutambulishwa kesho Jumatatu. Pia ameongeza kuwa video ya wimbo huo itafuata baadae.