BurudaniVideos

Sinaga Swaga inairudisha Hip Hop ya Bongo kwenye mstari wake – Young Killer

Rapper Young Killer anadai kuwa wimbo wake mpya, Sinaga Swaga umekuja kuirudisha ‘real hip hop’ kwenye mstari.

Amedai kuwa kipindi cha hivi karibuni rappers wengi wa Bongo wamekuwa wakilegeza ngoma zao ili kuvutia biashara, lakini yeye ameamua kukaza.

“Dhumuni la kufanya hii ngoma, nimetaka kuwaonesha kwamba hip hop yetu bado ipo na ina nguvu kubwa na ina uwezo wa kufika mbali zaidi ya hapo ambapo ipo endapo tutaendelea kuisupport na kuipa nafasi,” rapper huyo amemuambia mtangazaji wa Pride FM, Eddy Msafi.

Rapper huyo amesisitiza kuwa masikio ya mashabiki wa muziki Tanzania yanahitaji ngoma za aina ya Sinaga Swaga na si kupewa nyimbo za kuimba na kuchezeka tu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents