Tragedy
Simu za abiria waliopoteza maisha kwenye ajali ya ndege ya MH17 zinapokelewa na watu walioziiba
Familia za abiria waliopoteza maisha kwenye ajali ya ndege ya MH17 wanasema simu za wapendwa wao zinapokelewa na wezi waliozichukuia kwenye eneo ilipoangakua ndege hiyo nchini Ukraine.
Baadhi ya vitu vilivyosambaa baada ya ndege hiyo kudunguliwa na kuanguka
Ndugu hao waliopiga simu za wapendwa wao, wameliambia gazeti moja la Uholanzi kuwa simu hizo zinapokelewa na watu wenye lafudhi na sauti za watu wa Ulaya Mashariki.
Kuna taarifa pia kuwa mali za marehemu hao kama vile wallets, vito vya madini na vingine vimechukuliwa. Jana ilitangazwa kuwa siku ya maombolezo nchini Uholanzi na miili imesafirishwa huko ili kutambuliwa.