Burudani

Sikuwa najua pia kama Young Dee anatumia unga – Nyandu Tozi

Rapper Nyandu Tozi amesema yeye ni mmoja wa washkaji wa Young Dee ambao walipokea kwa mshangao taarifa yake kuwa alikuwa akitumia madawa ya kulevya.

Nyandu
Nyandu Tozi na Young Dee wakiwa na watangazaji wa kipindi cha XXL, Kennedy The Remedy, B12 na Adam Mchomvu

Amesema katika urafiki wao wote hakuwahi kumuona akitumia na kwamba amefurahi mno kuona kuwa ameachana nayo.

“Mimi kwangu nimefurahishwa na hilo lakini imekuwa surprise sana kwangu like damn! Yaani kwamba huyu young boy kumbe alikuwa anatumia hivi vitu pasipo mimi kujua,” Nyandu alimuambia mtangazaji wa Jembe FM, JJ.

“Unajua madawa ya kulevya ni tofauti na kinywaji kama bia au hard liquor kwamba sasa hivi ukiniuliza Young Dee anakunywa bia gani mimi najua kwasababu napokuwa naye namuona akiagiza, naiona ikiwa mezani. Hivyo vitu vingine hujui mtu anatumia muda gani,” ameongeza.

Kwa upande mwingine Nyandu naye amekanusha kutumia madawa ya kulevya. Amedai pia kuwa kuna ngoma mpya na Young Dee inakuja.

Msikilize hapo chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents