Burudani

Sijausikia wimbo wa Madee, watu wanasema mbaya – Nay wa Mitego

Jana Instagram ilitawaliwa na wababe wa Manzese, Nay wa Mitego na Madee ikiwa ni siku moja baada ya mkali wa Tip Top Connection, Madee kuachia wimbo mpya wa ‘Hela.’

Kwenye wimbo huo, kuna sehemu Madee anasIkika akisema, “yule kijana wa home sio staa, anatukana hata waliomzaa, wivu tamaa na njaa ukiendekeza ujue kidole utakaa,” mistari inayohisiwa kuwa imemlenga “Mmanzese” mwenzake, Nay.

Picha likahamia Instagram baada ya Nay kuandika “leo nimesikia wimbo mbayaaaaa kuliko nyimbo mbaya nilizowahi kusikia mwaka huu. Mtag huyo msanii mwenye huo wimbo kama ushausikia..?!

Hiyo ni post ambayo wachunguzi wa mambo walidai kuwa rapper huyo alijibu kiaina diss hiyo.
Nimepiga story na Nay kwenye Super Mega kutaka kujua kama ni kweli post ile ilikuwa ni njia ya kumjibu Madee.

“Wimbo wa Madee wenyewe mimi sijausikia mpaka saa hizi, labda itanishawishi je ni mbaya,maana watu wengi wameandika kwenye comments zao,”amesema Nay.

By Prince Ramalove (Kings FM)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents