Michezo
Shirikisho la soka Barani Ulaya UEFA yamsimamisha Mamadou Sakho
Shirikisho la soka Barani Ulaya UEFA,limetangaza kumsimamisha kwa siku 30 beki wa Klabu ya Liverpool Mamadou Sakho kwa ajili ya kuanza uchunguzi juu mchezaji huyo ambaye amegundulika kutumia madawa ambayo hayaruhusiwi michezoni.
Kitengo cha nidhamu na maadili cha shirikisho hilo kinataraji kuanza uchunguzi huo na baadaye kutangaza matokeo yake na adhabu.
Baada ya ushindi dhidi ya Manchester United Machi 17 katika Europa Ligi, Sakho,26, alipimwa na kuonekana kutumia madawa (Fat Burner) ambayo hayarusiwi katika michezo.
Raia huyo wa Ufaransa na kilabu yake walikubaliana kwamba hatoshiriki katika mechi yoyote hadi pale Uefa itakapokamilisha uchunguzi wake