Burudani
Shilole kuwarusha mashabiki wa Ubelgiji mwisho wa mwezi huu
Binti wa kinyamwezi mwenye sifa nyingi za uzuri na ustadi wa kuutumia mwili wake vizuri awapo jukwaani, Shilole anaumaliza mwaka 2014 vizuri kwa mashavu ya show za kimataifa.
Baada ya kuwarusha mashabiki wa Cape Town, Afrika Kusini weekend iliyopita, Shishi Bybye anatarajia kwenda kuwarusha mashabiki wake wa Ubelgiji mwishoni mwa mwezi huu.
Shishi atafanya show ya kwanza Nov.28 kwenye mji mkuu wa Belgium, jijini Brussels, ikifuatiwa na show ya pili Nov 29 itakayofanyika Hoeilaart.