Shetta: Sina tatizo na Hemedy, itakuwa alinielewa vibaya
Msanii wa muziki Shetta amesema hana tatizo lolote na Hemedy PHD, huku akidai kuwa huenda kauli yake aliyosema kwa sasa hatafanya collabo na wasanii wa ndani tena ilinukuliwa vibaya na huenda ndo imemsababishia matatizo hayo.
Hemedy PHD hivi karibuni baada ya kusikia kauli ya msanii huyo alitweet kuonyesha hakupendezwa na kauli hiyo.
MTU ANASEMA HATEGEMEI KUFANYA TENA COLLABO NA MSANII WA BONGO IKIWA NGOMA ZAKE ZOTE KABEBWA NA COLLABO!what a looseR!!thnk before you speak
— FAR AWAY (@hemedyPHD) November 10, 2014
Akizungumza na bongo5 leo, Shetta amesema kuwa kauli hiyo iliwakilishwa vibaya na vyombo vya habari.
“Nilichokisema katika project yangu mpya itakayo sitafanya collabo tena na msanii yoyote wa ndani kwa upande wangu ila kama kuna mtu anataka kufanya collabo na mimi milango ipo wazi, napenda kuweka wazi hili,nimeshafanya nyimbo sita nikiwa nimewashirikisha wasanii wa ndani, sasa huu ni wakati wa kutanua wigo kwa upande wangu, mimi binafsi sina tatizo na Hemedy, mimi nafikiri alinielewa vibaya tu, uwakilishaji wa habari katika vyombo vya habari waliwakilisha vibaya. Nitafanya collabo na mtu yeyote atakayehitaji kufanya na mimi kwenye project yake, lakini kwa wimbo nitakaotoa mimi either nifanye mwenyewe au nifanye collabo na msanii wa nje,” alisema Shetta.