Burudani
Shetta amrudisha producer Djobanjo
Baada ya kumfanyia kazi nzuri kwenye wimbo wake ‘Shikorobo’, Shetta ameamua kumrudisha Tanzania producer wa Comoro, Djobanjo kuja kumtengenezea ngoma nyingine.
Akiongea na E-News, Shetta amesema ameamua kumleta producer huyo nchini kwa mara nyingine.
“Unajua huwa nakubali sana mtu akifanya kazi nzuri. Najua watu wengi jina Djobanjo siyo geni. Imagine ilikuwa mimi ndio niende Comoro lakini kwakuwa ratiba yangu inabana nimeona nimlete aje tufanye project nyingine ambayo inafuata baada ya Shikorobo, soon wataisikia,” amesema Shetta.