Diamond PlatnumzVideos

Salome ya Diamond ni video ya muziki iliyotazamwa zaidi Kenya kwenye Youtube, Work ya Rihanna na Drake ni ya pili

Video ya wimbo wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Raymond, Salome, ndiyo video ya muziki iliyotazamwa zaidi kwenye mtandao wa Youtube nchini Kenya, kwa mujibu wa shirika la habari la BBC, kupitia takwimu ilizozipata.

15258620_1454017111294721_1203758597243142144_n

BBC Swahili wamedai kuwa kwenye orodha ya nyimbo 10 kutoka duniani kote, nyimbo za Tanzania zimetazamwa zaidi. Takwimu hizo zinadhihirisha jinsi ambavyo Wakenya wanapenda muziki wa Bongo Flava kuliko nchi nyingine yoyote ukitoa Tanzania yenyewe.

Hadi sasa, Salome ina views zaidi milioni 9.8 kwenye mtandao wa Youtube.

Hii ni orodha kamili:

Salome – Diamond Platnumz na Raymond
Work – Rihanna na Drake
Bado – Diamond Platnumz na Harmonize
Sauti Sol – Unconditionally Bae, na Alikiba.
Work from Home – Ty Dolla Sign na Fifth Harmony
This is What You Came For – Calvin Harris
Kwetu – Raymond
Cheap Thrills – Sia na Sean Paul
Pillow Talk – Zayn
Ain’t Your Mama – Jennifer Lopez

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents