Burudani

Sallam atangaza ujio wa tamasha la Diamonds Are Forever 2017

Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK aka ‘Fundi Mitambo’ ametangaza ujio mpya wa tamasha kubwa la Diamonds Are Forever 2017 ambapo safari hii litafanyikia katika uwanja wa Taifa.

Muimbaji huyo alifanya tamasha hilo kwa mara ya kwanza nchini mwaka 2012 katika ukumbi wa Mlimani City show ambayo ilihudhuriwa na watu wengi kwa kiingilio cha Tsh 50,000 na 100,000 kwa VIP.

Sallam akizungumza live na mashabiki katika mtandao wa Instagram (Insta Live) alisema show hiyo ipo kwenye maandalizi na itafanyika uwanja wa Taifa.

“Mjiandae na Diamonds Are Forever 2017, Diamonds Are Forever 2017 is back,” Sallam aliwaambia mashabiki.

Meneja huyo alidai safari hii tamasha hilo litafanyika uwanja wa taifa ili kuwapa fursa watu wengi zaidi ya kuhudhuria.

Hata hivyo hakuweka wazi ni lini au mwezi gani tamasha hilo litafanyika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents