Sallam aeleza majukumu yake kama meneja wa Diamond
Mmoja kati ya mameneja wa Diamond Platnumz, Sallam ameeleza majukumu yake akiwa kama meneja wa msanii huyo ambaye kwa sasa ana mafanikio makubwa ya kimuziki Afrika.
Akizungumza na Swahili Talk Radio ya nchini Denmark, Sallam alisema ingawa wote wamegawana majukumu lakini pia wanashirikiana katika maamuzi ya kila jambo.
“Hapa kuna meneja, kuna business meneja yaani wote tunashirikiana katika kila suala ambalo linaletwa kama ajenda ‘jamani mwaka huu 2016 tunafanyaje’ labda ajenda zipo 15, tunatakiwa tufanye tour, nyimbo tutoe ngapi na target yetu ni hii, goal yetu ni hii. Kwahiyo ni vitu ambavyo vyote vinawekwa juu ya meza na tunajadili,” alisema.
Msikilize zaidi hapo chini.
https://soundcloud.com/swahili-talk-radio/sallam-platnamz-meneja-interview-1