Picha

Salif Keita aiunga Mkono kampeni ya ‘Colour Kwa Face’ kutetea haki za albino

Kampeni ya msanii wa Kenya, Colour Kwa Face ya Nonini imeendelea kufanikiwa na kukua zaidi baada ya mwanamuziki na mwandishi wa nyimbo wa nchni Mali, Salif Keita kuiunga mkono.

1004831_456305784466780_602801773_n
Nonini akisalimiana na Salif Keita

526513_456303927800299_2131493001_n
Nonini na Salif Keita wakisikiliza jambo

Kampeni hiyo ina lengo la kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi na kupinga vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa.

555773_456303984466960_18770778_n

993369_456304031133622_64248301_n

1148899_456304071133618_488905192_n

Kampeni hiyo pia imeungwa mkono na kampuni ya Standard Group ambapo pamoja na mambo mengine, Nonini na watu wengine maarufu wameshiriki kwenye matembezi maalum.

1174873_455409324556426_1651104971_n

“Nimefurahishwa na kile kinachotokea Kenya. Afrika Magharibi hakuna makampuni yanayojihusisha kuunga mkono ualbino, hata vyombo vya habari,” alisema Keita kwenye makao makuu ya Standard Group.

1184900_456304154466943_544460444_n

1185457_456304034466955_1860969547_n

Source: Standard Media, Picha: Colour kwa Face Facebook Page

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents