Habari
Rose Ndauka ashirikishwa kwenye wimbo mpya wa TNG Squad ‘Crazy Man’
Wazee wa Ring on It, TNG Squad wamerejea tena kwa kishindo kizito huku wakipewa kick na producer aliyewatoa, P-Funk Majani wa Bongo Records. Wakali hawa wa nyimbo za dancehall na zinazochezeka, wamekuja na surprise!! Wamemshirikisha muigizaji wmahiri wa filamu nchini, Rose Ndauka.
Rose Ndauka (Picha: Imma Matukio)
Hata hivyo Rose hajaimba, bali amechombeza tu maneno matamu mwanzoni mwa wimbo huo uitwao Crazy Man. Na tunajua sababu ya Rose Ndauka kukubali kuweka sauti yake humo. Ni kwa sababu mchumba wake Malick Bandawe ni member wa kundi hilo, bila shaka ulikuwa haufahamu. Crazy Man ni wimbo mkali. Usikilize hapa.