Burudani
Road 2 MAMA: Show tatu kufanyika, Dar, Lagos na Durban
Kama bado unauchukulia poa muziki wa Tanzania, basi huu ni muda wa kufikiria upya na kubadili imani hiyo. Tanzania ipo vizuri kwenye ramani ya muziki wa Afrika na ndio maana mwaka huu pamoja na Diamond kutajwa kuwania tuzo za MTVMAMA 2014, Tanzania itakuwa mwenyeji wa show moja kati ya tatu za utangulizi wa tuzo hizo, Road to MAMA.
Show za Road to MAMA zitafanyika jijini Durban, Afrika Kusini, Lagos, Nigeria na Dar es Salaam,Tanzania, kulipigia promo tukio lenyewe la tuzo hizo litakalofanyika June 7.
Kwenye show hizo wasanii waliotajwa kuwania tuzo hizo za mwaka huu watakuwepo pamoja na wasanii ma madj wanaofanya vizuri kwenye nchi husika. Show hizo katika kipindi cha mwezi huu hadi May.