Bongo Movie

RJ Company ya Ray Kigosi na Johari inakuja na tamthilia mpya ya runinga

Wasanii wa filamu wanaounda kampuni ya RJ Company, Brandina Chagula ‘Johari’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ wanajiapanga kuingia kwenye biashara ya kuandaa tamthilia ambazo zitakuwa zinaonyeshwa katika runinga.
johari2

RJ Company ni miongoni mwa kampuni kongwe za filamu nchini ambazo mpaka sasa imeshaandaa filamu nyingi pamoja na kuibua vipaji vipya vya waigizaji.

Akizungumza katika kipindi cha Uhondo cha EFM, mmoja kati ya wakurugenzi hao, Johari Chagula, amezungumzia mipango mbalimbali ya kampuni hiyo.

“Kwa sasa bado tunaendelea kutoa filamu kama kawaida ila tunampango mkubwa zaidi, kuna tamthilia ya runinga ambayo inakuja, kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kula,” alisema Johari.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents