Burudani
Rita Ora ana ‘bwana’ mpya, ni huyu jamaa (Picha)
Kuna couple mpya nchini Marekani.
Imebainika kuwa Rita Ora na mpiga drums maarufu, Travis Barker wana uhusiano wa kimapenzi. Wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza kwenye mechi ya kikapu ya mastaa iliyoandaliwa Power 106 wiki chache zilizopita huko Los Angeles.
“Me and the beautiful @ritaora at @power_106 #Power106AllStars,” Barker aliandika kwenye picha aliyoweka Instagram wiki iliyopita.
Rita aliirepost picha hiyo na kuandika “nice to see you too.”
Na sasa imebainika kuwa wawili tayari ni wapenzi. Msemaji wa Barker amethibitisha taarifa hizo.
Kabla ya Travis, Rita amewahi na mtoto wa Tommy Hilfiger, Ricky Hilfiger Calvin Harris na Rob Kardashian.