Burudani
Rihanna kuigiza filamu mpya ya James Bond
Kuna tetesi kuwa Rihanna ataigiza kwenye filamu mpya ya James Bond, ‘Bond 24.’
Kwa mujibu wa mtandao wa HollywoodLife, Rihanna atakuwa na uhusika mdogo kwenye filamu hiyo na maongezi kati yake na waandaaji yanaendelea.
Chanzo kimoja kimeuambia mtandao huo kuwa Rihanna ataonekana kwenye sehemu chache tu na kuna uwezekano akaimba wimbo kwenye filamu hiyo.