Rihanna amuunga mkono Kanye West aliyetangaza kuwania urais wa Marekani 2020
Kanye West alitangaza uamuzi mkubwa kwenye VMAs weekend iliyopita – kuwania urais wa Marekani 2020.
Haijalishi kama ataendelea na uamuzi huo, lakini tayari rapper huyo ameshapata support kutoka kwa mastaa wengine akiwemo Rihanna.
Kwenye interview na ET, muimbaji huyo wa “Bitch Better Have My Money”alimuunga mkono Yeezy. “I mean people are voting for [Donald] Trump,” alisema Rihanna. “Who wouldn’t vote for Kanye?!”
Kwa upande mwingine Rihanna aliisifia hotuba ya Kanye West.
Naye msanii wa Uingereza, Leona Lewis amedai kuwa ni shabiki wa Kanye ambapo pamoja na kusifia hotuba yake amefanya cover ya wimbo wake Only One.
I was quite moved by @kanyewest speech at the VMA's. In light of this, I would like to share this with you… https://t.co/tFkQ8h9GFf
— Leona Lewis (@leonalewis) September 1, 2015