Burudani

Rich Mavoko asainishwa na kampuni ya usimamizi ya Kenya inayomsimia pia Avril

Rich Mavoko amesaini mkataba na kampuni ya usimamizi ya Kenya iitwayo Kaka Empire iliyoanzishwa na rapper Rabbit.

10632697_823237051049400_2549191303913228859_n

Kampuni hiyo pia inawasimamia wasanii wa Kenya akiwemo Avril, Raj, FemiOne na Owago.

Mavoko ameiambia Bongo5 kuwa kampuni hiyo itakuwa ikisimamia kazi zake zote kwa upande wa Kenya peke yake.

11008219_867236613352077_1669615294_n

Amedai kuwa uamuzi wa kuamua kuwa chini ya kampuni hiyo umekuja baada ya kubaini kuwa ana mashabiki wengi nchini Kenya na kuna watu wamekuwa wakifaidika kwa kuuza kazi zake bila yeye kufahamu.

“Nimekuta mdundo.com kuna mtu anachukua hela zangu tangu miaka mitatu nyuma, tangu nyimbo ya Silali. Sio hela ndogo, ni dola kadhaa. Yule jamaa alienda kujitambulisha kwamba yeye ni meneja wangu,” amesema Mavoko.

“Kwahiyo jamaa wakaniambia kwamba hakuna mtu anayeweza kufuatilia vitu vyako vya Kenya kwahiyo inabidi upate wakala au mtu anayeweza akasimamia kazi zangu za Kenya naye atakuwa anachukua asilimia lakini haki zako zote unazipata,” ameongeza.

10959079_1575420532745168_1897171893_n
Rich akiwa na Rabbit

Hivi karibuni Rabbit aka Kaka Sungura alimshirikisha Mavoko kwenye wimbo wake ‘Njoo’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents