Rich Mavoko akanusha kufichwa ndani na mwanamke
Rich Mavoko amedai kuwa ukimya wake hautokani na kufichwa ndani na mwanamke kama baadhi ya watu wanavyoamini.
Akizungumza na E-Newz ya EATV jana, Mavoko alisema yeye binafsi hapendi hapendi kuweka sambamba muziki na maisha yake ya uhusiano.
“Kukaa kimya inategemea na kitu unachotaka kutoa. Muziki umekuwa biashara na ni biashara ya kujipanga,” alisema. “Kukaa kwangu kimya sina maana sina kazi ndani. Mimi ni mtu mzima siwezi nikasema kazi yangu niingize na mapenzi, itakuwa ni vitu viwili tofauti. Mambo yangu ya kawaida siwezi kuchanganya na muziki.”
“Halafu kusema mwanamke anaweza kunibana kwenye mambo yangu ya muziki huo ni uongo. Watu wanalalamika sana kwenye mitandao yangu ya kijamii kuhusu kazi, wanipe time, kwenye mwezi wa kumi mwishoni au mwezi wa 11 mwanzoni kazi mpya itatoka,” aliongeza staa huyo.