Remix ya Piga simu ya Diva na Ommy Dimpoz yapigwa chini
Unakumbuka tuliwahi kuandika mipango ya yule mtangazaji wa Clouds FM wa kipindi cha Ala za Roho, Loveness aka Diva ya kuifanyia remix ngoma yake ya Piga Simu? So the remix is done but ……… something is amiss!
Inadaiwa kuwa timu inayohusika na upitishaji wa ngoma kwenye kituo hicho cha radio imeigomea ngoma hiyo kwa kudai kuwa hakukuwa na haja ya kuendelea kuwepo sauti za Diamond kwenye remix kwakuwa ni sawa na kuongeza jojo mdomoni kuipa utamu ile iliyokwisha utamu tayari.
Hata hivyo rumor has it kwamba uamuzi huo haujamfurahisha Ommy Dimpoz ambaye anajisikia kama kakosewa heshima hivi!
So timu hiyo imependekeza kuwa sauti za Diamond zitolewe halafu watafutwe wakali wengine wakuinogesha zaidi remix hiyo na kuipa support sauti ya Ommy ambayo tayari imeshaingizwa.
Timu hiyo inayoongozwa na Peter Moe, Kerry , Dj Too short na Team Makorokocho imependekeza beat ibadilishwe na aongezeke rapper Fid Q ambaye wanahisi mashairi yake yataongeza uzito na umakini wa remix hiyo.
The question is!!! Fid Q atakubali? Tunajua hawezi kukataa whether he likes or not sababu going to war with Clouds FM can ruin his career. Unakumbuka ile saga ya Fid Q aliposhushwa stage kwenye Fiesta alipopanda kuperform ngoma waliyofanya na TID several years ago? Yeah the beef almost killed his career lakini waliyamaliza kiume!