Michezo
Real Madrid bado wanataka kumng’oa De Gea Man United
Golikipa namba moja wa klabu ya Manchester United, David De Gea bado anahitajika na klabu ya Real Madrid kwa mujibu wa tovuti ya Hispania Don Balon imedai kuwa bosi wa Real Madrid Zinedine Zidane amemfanya David De Gea kuwa nambari moja kati ya wachezaji anaotaka kuwasajili majira ya joto.
De Gea amekuwa kipenzi cha mashabiki wa United alikaribia kutua Madrid 2015 lakini alibakia Old Trafford. Amekuwa mchezaji bora wa msimu kwa United miaka mitatu mfululizo.