Diamond PlatnumzVideos

Raymond asimulia jinsi alivyomshawishi Diamond hadi kumchukua WCB (Video)

Raymond amesimulia jinsi ambavyo alimshawishi Diamond hadi kuamua kumchukua kwenye label yake, WCB.

12960178_1004660659627506_1027037883_n

Ameiambia Bongo5 kuwa alipigiwa simu na mshkaji wake, Maromboso aende studio kuungana naye katika kusikiliza wimbo wa Diamond aliokuwa anataka mawazo ya watu wengi.

“Brother Diamond akifanya ngoma anapenda management yake, kuanzia madancer, mameneja wote waweze kusikiliza wimbo wake. Katika hiyo crew ya watu waliokuwepo Maromboso akapendekeza na mimi niwepo,” amesema.

Anasema baada ya kumshauri vitu kadhaa Diamond aligundua ana kitu cha ziada na kumuuliza kisa cha kutotoka hadi muda huo. Amedai kuwa Diamond alimuomba nyimbo zake azisikie na akawa anamshauri vitu vya kurekebisha. Aliendelea kurekodi nyimbo kwenye studio mbalimbali na kuwa anamtumia hadi alipofungua studio ya WCB.

Anasema kuwa kwenye studio hiyo alirekodi nyimbo nyingi kali zilimchanganya Diamond na uongozi wake hadi wakashindwa watoi upi.

Ray ameongeza kuwa Bado ilitoka kwa mbinde kwakuwa kulikuwa na nyimbo zingine kali sana. Mtazame hapo juu kumsikia akielezea.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents