Burudani

Ray J adai ‘uchizi’ wa Kanye West unakaribia kuuvunja uhusiano na mchumba wake

Ray J hajapenda kuwekwa kwenye video ya wimbo Famous wa Kanye West.

RAY-J-and-Kim-K

Kwenye video hiyo Ray J aliyewahi kuwa mpenzi wa Kim Kardashian, anaonekana akiwa mtupu amelala kitandani na mastaa wengine. Akiongea na Entertainment Tonight kwenye tuzo za BET, Ray J alisema alishangaa kuwepo kwenye video hiyo na hataki hata kuisikia.

“Don’t put me part of nothing that’s weird, that don’t make sense,” alisema. “Can I grow up?”

Ray J pia alisema kuwa mchumba wake, Princess Love, amechukizwa mno na video hiyo. “I’m engaged. My marriage is all messed up ‘cause of craziness. I’m not part of nothing crazy,” alisema Ray J.

“I walk down a good path. My fiancée tripping. It’s all bad in my world, and that ain’t cool.”

Kabla Kanye na Kim kuwa pamoja, Ray aliwahi kuwa na uhusiano na Kim mkanda wao maarufu wa ngono ulivuja mwaka 2007.

Kwenye video ya Famous, West amemweka pia ex wake Amber Rose, pamoja na mastaa wengine wakiwemo Taylor Swift, Rihanna, Chris Brown.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents