Burudani

Ray C: Nina uhakika Alikiba akipata support ya Diamond anaweza kufika mbali

Ray C ambaye siku chache zilizopita ameachia wimbo mpya baada ya kimya cha muda mrefu, ameweka wazi kile anachotamani kukiona baina ya wasanii wawili wenye mashabiki wengi Tanzania, Alikiba na Diamond.

Ray C

“Wenzetu wasanii wa Nigeria wanashirikiana kwa kila hali na ndio maana wanafika mbali,” alisema Ray C kupitia Clouds TV. “ Wasanii wa Tanzania hatuna hiyo, yaani mtu kama Diamond anatakiwa awe karibu na Kiba sio kwa upinzani wa biashara lakini kama mtu na kaka yake kwamba huyu alitangulia, na anamjua kwamba ni mkali .”

Aliendelea,

“Napenda siku moja nimsikie Diamond na Kiba wanafanya kazi pamoja, Ray C na Recho wanafanya kazi pamoja Ray C na Jay dee wanafanya kazi pamoja, tukienda hivyo ndio tutafika mbali, lakini tukitengeneza upinzani team nani team nani hatuwezi kufika sehemu yoyote, sababu ule muda ambao unafikiria kuzozana na kuangalia mashabiki wanasema nini ndio ungeutumia ule muda nyie wote wawili kufanya kazi kwa pamoja.”

“So I think kila mtu ana nafasi yake, Alikiba is a very very good singer, aangalie labda ni management tatizo au ni nini ili aweze kurudi kwenye peak tena…Lakini nauhakika alivyorudi sasa hivi akipata support hata ya huyo Diamond mwenyewe anaweza kufika mbali.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents