Mshambuliaji kinda wa Manchester United, Marcus Rashford yupo mbioni kusaini mkataba na kampuni ya utengenezaji wa vifaa vya michezo, Nike.
Mpaka sasa Rashford amebakisha miezi 14 mkataba wake na Manchester United ambao anapokea mshahara wa paundi 15,000 na bonansi ya paundi 5,000 anatarajiwa kupewa mkataba mkubwa zaidi.
Rashford ameshaifungia timu yake ya Manchester United jumla ya magoli saba tangu alipoanza kuingia kwenye kikosi hicho kwenye mechi ya kwanza ya kombe la Uefa dhidi ya Midtylland ambapo alifunga magoli mawili kwenye ushindi wa magoli manne walioupata Manchester United.
Mchezaji huyo ambaye anawaniwa na kampuni ya Roc Nation Sports inayomilikiwa na staa Jay Z pamoja na wakala maarufu duniani Jorge Mendez.