Tragedy
Rais wa Zambia Michael Sata afariki dunia
Rais wa Zambia, Michael Sata amefariki dunia. Alikuwa amelazwa kwenye hospitali jijini London, Uingereza.
Sata amefariki Jumanne hii baada ya kulazwa kwenye hospitali ya King Edward VII. Alikuwa na umri wa miaka 77.
Nafasi ya Sata inaweza kushikwa kwa muda na waziri wa ulinzi Edgar Lungu, ambaye hivi karibuni alikuwa kaimu rais ama makamu wa rais Guy Scott, ambaye atakuwa rais wa kwanza mzungu tangu FW de Klerk wa Afrika Kusini mwaka 1994.