Habari

Rais wa zamani wa Marekani George H.W. Bush alazwa hospitalini

Rais wa zamani wa Marekani, George H.W. Bush amekimbizwa katika hospitali ya Houston Methodist ya mjini Texas baada ya kuzidiwa ghafla.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na mkuu wa wafanyikazi wa rais huyo wa 41 wa nchi hiyo, Jean Becker kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na kuna uwezekano mkubwa akaruhusiwa kutoka hospitalini siku chache zijazo.

Siku chache zilizopita mtoto wake George W. Bush ambaye na yeye aliwahi kuwa Rais Marekani alitoa ripoti kuwa atahudhuria sherehe za kuapishwa Donald Trump huku akiongeza kuwa baba yake, George H.W., hatohudhuria kutokana na umri wake kuwa umeenda sana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents