Habari
Rais Magufuli ampongeza Donald Trump kwa kushinda urais Marekani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, amemuandikia ujumbe wa kumpongeza Rais mpya wa Marekani Donald Trump baada ya kushinda na kuwa rais mpya wa nchi hiyo.
Rais Magufuli amemuandikia ujumbe huo katika mtandao wa Twitter kutoa hongera zake kwa kiongozi huyo aliyekuwa akishindana na Hillary Clinton wa chama cha Republican.
Donald ameshinda majimbo ya uchaguzi 276, huku Clinton akishinda 218.
BY: EMMY MWAIPOPO