Burudani
Rachel (Kizunguzungu) akanusha tetesi za kuwa anatumia dawa za kulevya
Msanii kutoka THT Rachel amekanusha tetesi za kuwa ameanza kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya (unga na bangi).
Akizungumza na bongo5 leo, Rachel amesema kitendo cha kuzushiwa kimemuumiza sana.
“Kuna wimbo nilikuwa nafanya na TID, hakuna ukweli wowote kwamba nilikuwa natumia madawa, dah sitaki hata kuzungumzia hayo maswala kabisa. Nawaambia Watanzania na wadau wa muziki kuwa hilo swala halikuwa na ukweli wowote, cha msingi wafuate kazi zangu waachane na vitu ambavyo havina ukweli wowote” Alimaliza.