Ni yule mrembo wa kitanzania ambaye anaiwakilisha nchi katika shindano la kumsaka Miss Africa United States, shindano lililoshirikisha wanafunzi wa kiafrika wasomao huko marekani.
Ni yule mrembo wa kitanzania ambaye anaiwakilisha nchi katika shindano la kumsaka Miss Africa United States, shindano lililoshirikisha wanafunzi wa kiafrika wasomao huko marekani.
Rachel ambaye ni mdogo wake Miss Tanzania 1999 Hoyce Temu alipata tiketi hiyo baada ya kushinda taji la Miss Africa California 2007 mapema mwaka huu.
Rachel anashindana na warembo wengine wapatao 18 kutoka nchi tofauti ikiwepo Congo, Senegal, Nigeria, Kenya, Sierra Leon, Uganda, Cameroon, Gambia, Ethiopia, Zambia, Afrika ya Kusini, Burundi, Liberia, Burkina Faso, Sudan, Ghana na Guinea.
Ili kumchagua Rachel kongoli humo http://www.missafricaunitedstates.com/mausa/vote.htm ambapo utaona picha za warembo wote na chini yake unaichagua Tanzania na kukong’oli Vote.
Shindano hilo linatarajiwa kufanyika Novemba 3 hivyo Shime Shime Watanzania…..Tumtoe kimaso maso Rachel aweze ipeperusha bendera ya TZ.